“Licha ya matatizo yanayotokea tunapaswa kujua kwa imani kwamba Mungu asiyeonekana na mwenye nguvu bado yuko kwenye kiti chake cha enzi, akisimamia kila kitu kinachoendelea, huku akijua bayana kwamba mapenzi yake lazima yatimie, bila kujali watu wasiomwamini wenye upofu wa rohoni.”

“ATP inaweza kukusaidia kupata akili na nguvu ya kufanya jambo ambalo katika hali ya kawaida lisingewezekana. Wakati mwingine unaweza kufanya jambo hata wewe mwenyewe ukashangaa umelifanyaje. Unaweza kwa mfano kufukuzwa na mnyama mkali ukapenya mahali ambapo, katika hali ya kawaida usingepenya. Sasa usishangae tena. Kilichofanya upenye ni ATP.”