“Mungu anataka tujifunike kwa ngao yake. Yaani, tuwe na imani iliyokomaa katika Bwana na yeye atatufunika. Maana ya kauli hiyo ni kwamba kila kiungo cha miili yetu kuanzia unyayo hadi kichwa lazima kifunikwe kwa silaha ya Mungu, ambayo Mungu anaiita panoplia. Panoplia haimo katika kamusi ya Kiswahili au Kiingereza, lakini maana yake ni ‘ngao kamili ya Mungu’. Hii si tu silaha ya Mungu. Ni silaha kamili ya Mungu tunayotakiwa kujifunika kwayo.”

“Licha ya matatizo yanayotokea tunapaswa kujua kwa imani kwamba Mungu asiyeonekana na mwenye nguvu bado yuko kwenye kiti chake cha enzi, akisimamia kila kitu kinachoendelea, huku akijua bayana kwamba mapenzi yake lazima yatimie, bila kujali watu wasiomwamini wenye upofu wa rohoni.”

“Ukiitwa mtoto kidini ina maana una imani na unyenyekevu mbele ya Mungu, kama ambavyo mtoto ana imani na unyenyekevu mbele ya mzazi wake. Lakini ukiitwa mtoto kidunia watu watakudharau.”

“Ukikasirika, aliyesababisha ukasirike ni Shetani aliyeko ndani yako; na ukiwa na furaha, aliyesababisha uwe na furaha ni Mungu aliyeko ndani yako.”

“Ukimheshimu baba au mama yako katika mambo mema au mabaya umemheshimu Mungu katika mambo mema.”

“Wenye mamlaka wana dhamana za mamlaka zao kama watumishi wa Mungu, kwa sababu Neno la Mungu liko wazi kwamba Mungu ndiye aliyewapa mamlaka hayo.”

“Kuwa na kiasi katika matarajio yako. Hatuna uwezo wa kuona mambo kama Mungu anavyoyaona.”

“Kulingana na muda wa Mungu, maisha ya Adamu yalikuwa siku 0.93 au saa 22:32! Maisha ya mwanadamu ni siku 0.07 au saa 1:68!”

“Kama miaka 1000 ya duniani ni sawa na siku moja ya Mungu; hivyo basi, miaka 930 aliyoishi Adamu ni sawa na siku 0.93 au saa 22:32 za Mungu. Kwa hiyo, ili siku ya Mungu itimie Adamu alipaswa kuishi miaka 70 (siku 0.07 au saa 1:68) zaidi! Ukiidadavua saa 1:68 unapata saa 2:08. Kulingana na muda wa mbinguni tunapaswa kuishi kwa muda wa saa 2:08! Muda huo ni mfupi sana.”

“Ukijidharau unadharau uwezo ambao Mungu alikuwekea ndani yako.”